News

Find what's going on with us

Steps Tanzania yatoa mafunzo kwa Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii (CHW) juu ya kutoa huduma na kupambana na Magonjwa ya UVIKO 19 na Kifua Kikuu.

Katika kutekeleza Mradi wa C19RM unaofadhiliwa na Global Fund Kupitia kwa Amref Health Africa in Tanzania @amreftz , Steps Tanzania imetekeleza afunzo hayo kwa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (CHW) katika Wilaya za Bariadi CC, Bariadi DC, Maswa , Busega, Meatu na Itilima za Mkoa wa Simiyu huku Dodoma CC, Chamwino na Chemba kwa Mkoa wa Dodoma.

Mafunzo hayo yaliwawezesha CHW kutambua uhusiano na tofauti zilizopo kati ya magonjwa ya UVIKO 19 na TB pamoja na kujua njia mbali mbali za kuenea kwake ambazo kwa asilimia kubwa hufanana.

Pia waliweza kujengewa uwezo juu ya mbinu/ namna mbalimbali za kutatua changamoto zinazoibuka katika jamii kipindi wanapofanya uhamasishaji na utoaji wa elimu juu ya chanjo ya UVIKO 19.Katika kutekeleza Mradi wa C19RM unaofadhiliwa na Global Fund Kupitia kwa Amref Health Africa in Tanzania @amreftz , Steps Tanzania imetekeleza afunzo hayo kwa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (CHW) katika Wilaya za Bariadi CC, Bariadi DC, Maswa , Busega, Meatu na Itilima za Mkoa wa Simiyu huku Dodoma CC, Chamwino na Chemba kwa Mkoa wa Dodoma.

Mafunzo hayo yaliwawezesha CHW kutambua uhusiano na tofauti zilizopo kati ya magonjwa ya UVIKO 19 na TB pamoja na kujua njia mbali mbali za kuenea kwake ambazo kwa asilimia kubwa hufanana.

Pia waliweza kujengewa uwezo juu ya mbinu/ namna mbalimbali za kutatua changamoto zinazoibuka katika jamii kipindi wanapofanya uhamasishaji na utoaji wa elimu juu ya chanjo ya UVIKO 19.

Baada ya mafunzo kukamilika timu za CHW ziliahidi kuongeza matokeo hususan kwa chanjo dhidi ya UVIKO 19 kwa kuhamasisha watu kuchanja pamoja na kuwaibua watu wenye TB, huku wakiwashukuru wadau na Serikali kwa Elimu waliyoipata